Monday, September 7, 2015

Anonymous

Ujue Undani wa Biashara ya Mnadani!

madini
NI Jumatatu nyingine tena napenda kukukaribisha katika safu hii maalum ya Ujasiriamali.
Wiki iliyopita tulizungumzia namna ya kuanzisha biashara ya genge hivyo kuwaamsha walioamini kuwa hawawezi, leo nitazungumza nanyi wasomaji wangu kuhusu biashara ya kuzunguka minadani.
MNADA NI NINI?
Hii ni sehemu maalum iliyotengwa na sekta husika, wananchi au wanakijiji wa sehemu husika kwa ajili ya wafanyabiashara wa bidhaa tofauti na wanaotoka sehemu mbalimbali kwa ajili ya kufanya biashara zao.
KWA NINI MNADANI?
Kwa kuwa mnadani kunakutanisha wafanyabiashara wa sehemu na bidhaa mbalimbali, hata bei za bidhaa hizo hutofautiana na hivyo hufanya kukutanisha idadi kubwa ya watu kama wateja na wafanyabishara.
Biashara ya mnadani ni biashara nzuri kwa mtu anayetaka kukuza mtaji wa biashara yake, kwa kuanza na mtaji mdogo kwa kuzungusha kwenye minada mbalimbali mwisho wa siku unaweza kuongeza mtaji na kuwa mkubwa kama utakuwa tayari katika kuzunguka minada hiyo.
Biashara ya mnadani inakuwa na uhakika kutokana na bidhaa uliyopeleka kwa walaji wako, kama utakuwa na uwezo wa kupeleka dagaa kwa wahitaji wa dagaa ni dhahiri utaweza kufanya biashara hiyo vizuri zaidi kwa sababu wateja wako ni wahitaji wa bidhaa yako.
UZURI WA BIASHARA YA MNADANI
Inakupa fursa ya kuzunguka maeneo mengi ya wilaya au mkoa husika au nchi husika, kufahamiana na watu mbalimbali sambamba na kubadilishana uzoefu na ujuzi wa biashara yenu.
UPATIKANAJI WA FURSA MPYA
Kwa kuzunguka sehemu mbalimbali minadani, kama wewe ni mjasiriamali mwenye malengo ya kufanikiwa katika maisha yako, unaweza kupata fursa nyingi sana uwapo njiani ukielekea maeneo ya minadani, hata kama siyo muda huo lakini ipo siku unaweza kuwekeza au kufanya biashara kwa kutumia rasilimali ya aridhi au eneo ulilodhamiria.
AINA ZA BIASHARA KATIKA MINADA
Zipo aina nyingi za biashara ambazo unaweza kuzifanya kwa kuzunguka kwenye minada.
Mojawapo ni biashara ya nguo za mitumba.
Tukutane wiki ijayo tuangalie sehemu ya pili ya mada hii kwa ajili ya wajasiriamali.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.