Thursday, August 27, 2015

Anonymous

MKAPA Anguruma Tena, LOWASSA Visingiki Kila Kona, NEC Yashitukia Vyama Vya Siasa, + UKAWA Yafanyiziwa! (Audio)

Kama hukuwa karibu na radio yako asubuhi hii uchambuzi wa magazeti @CloudsFM utakuwa umekupita. Zimesikika kubwa za leo kwenye vichwa vya habari baadhi zikiwa.. 

Vyama vya Siasa mtegoni, ratiba ya kampeni ya zua mjadala… UKAWA wafanyiziwa wakwama kupata uwanja wa Jangwani, NEC yapiga marufuku kampeni za mikusanyiko, Lowassa vizingiki kila kona azuiliwa kutumia uwanja wa Jangwani. 

Mkapa anguruma tena alibariki Lowassa kukatwa, mgombea Urais CCM John Magufuli arudisha matumani kwa Watanzania asema akipewa nafasi ya kuiongoza nchi atateua Serikali yenye Mawaziri watakao kuwa watendaji kazi na waadilifu. 

Mgombea Urais kupitia CHADEMA Edward Lowassa kuongea na wanawake wa katika kongamano la Wanawake lililoandaliwa na BAWACHA ya CHADEMA leo… Walemavu wasema CCM wanawabagua, Chama cha ACT Wazalendo kimetangaza kuzindua kampeni za uchaguzi tarehe 30 mwezi huu. 

Sumaye awa guzo CCM, NEC yashitukia, yasema kila Chama kifuate ratiba watoa angalizo kwa vyama hivyo kufuata Sheria zinazohusiana na namna na utaratibu wa kufanya kampeni hizo.
Sauti ya uchambuzi wa magazeti kupitia #PowerBreakfast ipo hapa chini.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.