AY amewachukua Hermy B na Marco Chali kutengeneza ngoma yake mpya.
AY ameshare picha hiyo juu akiwa studio na watayarishaji hao wakubwa
nchini wanaowakilisha studio maarufu zaidi, Hermy B wa B’Hits na Marco
Chali wa MJ Records.
Hiyo itakuwa ni mara ya kwanza AY anakutana tena studio na Hermy B
baada ya kuwahi kupishana katika masuala ya kibiashara mwaka 2012.Baada
ya hapo AY amekuwa akifanya kazi zaidi na Marco.
“Unategemea kitu kitatokaje?? Best Producers @marcochalitz &
@hermyb kwenye chumba kimoja na Mzee wa Commercial.. BIT TINGZ R GWAN!!
#ZEE #ElCapo #FAYAAAA #KofiazaMarcoChali,” ameandika AY.
Mashabiki wameonesha kufurahishwa mno na picha hiyo na matarajio yao ni makubwa.

Note: Only a member of this blog may post a comment.