Saturday, September 12, 2015

Anonymous

TAMBWE Anasubiri Kuipiga Coastal Nne Zake!

AmissTambwe2.jpgKESHO Jumapili, Yanga itaanza harakati zake za kutetea ubingwa wa Ligi Kuu Bara kwa kucheza mechi ya kwanza dhidi ya Coastal Union kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam huku straika wake, Amissi Tambwe akitaka pia kutetea rekodi yake.
Msimu uliopita Coastal Union yenye maskani yake Tanga ilifungwa mabao 8-0 na Yanga huku Tambwe raia wa Burundi akifunga mabao manne peke yake, hivyo anachotaka ni kuendeleza rekodi hiyo.

Akizungumza na Championi Jumamosi, Tambwe aliyekuwa mfungaji bora wa ligi kuu msimu wa 2013/14, alisema amejipanga vizuri kuhakikisha anaitungua Coastal na kuendeleza rekodi yake.
“Nashukuru Mungu nilifanya vizuri wakati ule, sasa nimejiandaa vizuri kufanya tena kama vile nilivyofanya ili kutetea rekodi yangu, ujue kufunga mabao manne katika mechi moja si jambo dogo. 

“Najua kuna ushindani mkubwa kuanzia ndani ya timu hadi uwanjani unapopambana na wapinzani wako lakini nimepania kufanya vizuri na kuifikia rekodi yangu dhidi ya Coastal,” alisema Tambwe.
Msimu uliopita Tambwe alifunga mabao 14 huku mfungaji bora Simon Msuva wa Yanga akifunga mabao 17.Alipokuwa mfungaji bora, Tambwe alifunga mabao 19.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.