Madee amesema hajalitupilia mbali suala la kumrudisha Dogo Janja shule.
Hata hivyo amesema anachoangalia kwa sasa ni ujio wa ngoma yake [Dogo Janja] mpya.
“Sitaki kusema eti nimeamua kukauka moja kwa moja asirudi shule,”
alikiambia kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio wiki hii. “Vipo vingi
ambavyo sasa hivi anaviongelea, ambavyo vipo kwenye plan, lakini kikubwa
kabisa nilikuwa na plan nitoe ngoma yake and then mwakani atafanya
anachokitaka hata ukimpigia atasema anachotaka.”

Note: Only a member of this blog may post a comment.