Jaji Mkuu wa Shindano la Bongo Star Search 2015 (BSS), Rita Paulsen ‘Madam Rita’
Na Hamida hassan
Jaji Mkuu wa Shindano la Bongo Star Search 2015 (BSS)
linaloendelea hivi sasa, Rita Paulsen ‘Madam Rita’ amewapiga chini
wanasiasa waliokuwa wakitamani awe nao na kusema kuwa yeye ni
mfanyabiashara hivyo hawezi kusapoti chama chochote cha siasa.
“Mimi ni mfanyabiashara, kujikita na siasa kiukweli siwezi ila siyo
kama sijajiandikisha, nina ‘kichinjio’ changu na Oktoba 25 nitampigia
kura yule ninayeona anafaa kuliongoza taifa letu ambaye kwa sasa ni siri
yangu,” alisema Madam Rita.

Note: Only a member of this blog may post a comment.