Mengi yamesemwa kuhusu picha za mtandaoni za Zari akimpa mtoto wake
maziwa ya chupa, wengi wao hasa wanawake wakimlaumu kwa kushindwa
kumnyonesha maziwa yake.
Mama huyo wa mtoto wa superstar wa Afrika Mashariki Diamond Platnumz, Tiffah amemjibu shabiki mmoja wa kike aliyemuuliza kwanini hamnyonyeshi Tiffah maziwa yake.
Zari alimjibu kwa picha akiwa anamnyonyesha Tiffah na kuandika; “Nini kinakufanya ufikirie simnyonyeshi…unasoma mambo mengi kutoka kwenye vyombo vya habari.”

Note: Only a member of this blog may post a comment.