Monday, June 15, 2015

Anonymous

LOVE YA UKWELI: [PICHAZ] VIKONGWE WA MIAKA ZAIDI YA 100 WAFUNGA NDOA, WALIKUWA WACHUMBA MIAKA 27 -PICHAZ

Nani amesema umechelewa kuoa au kuolewa? kuna watu huwa na wasiwasi kuwa wamechelewa kufunga ndoa kwa madai umri umekwenda lakini kwa George Kirby na Doreen Luckie imekua tofauti kabisa baada ya kuamua kufunga ndoa wakiwa na umri mkubwa.

George mwenye miaka 103 na Doreen mwenye miaka 91 waliamua kutimiza ndoto yao hiyo ya siku nyingi kwa kufunga ndoa.

Wawili hao wamefunga ndoa baada ya kuwa kwenye uhusiano kwa miaka 27 huku kila mmoja akisema hajutii kuchelewa kufanya maamuzi hayo.

Sherehe hiyo ya aina yake ambayo ilifanyika katika hotel ya Eastbourne, Kusini mwa Uingereza ilihudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo ndugu na marafiki wa karibu wa familia hiyo.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.