Monday, September 7, 2015

Anonymous

MAAJABU YA JIJI LA DAR...KWELI DUNIA INA MAMBO!

Boniphace Ngumije
Skendo! Mpangaji aliyejitambulisha kwa jina la Mama Alex, mkazi wa Survey Mwenge, jijini Dar, anadaiwa kutifuana na mama mwenye nyumba yake, Georgina Zamani kwa madai ya ushirikina.
Uchawi (4)-001 
Mama mwenye nyumba, Georgina Zamani.
Habari kutoka nyumbani hapo zilidai kwamba, kufuatia ishu hiyo, baba mwenye nyumba, Pius Zamani ameisusa familia yake kutokana na madai hayo dhidi ya mkewe anayetuhumiwa kwa ulozi.
Akizungumza na gazeti hili, Georgina alisema matatizo kati yake na mumewe yalianza baada tu ya mpangaji huyo kuhamia nyumbani kwake hapo miaka mitatu iliyopita.
Alidai kwamba, jambo lililomshangaza ni jinsi mpangaji huyo anavyoishi kwenye nyumba hiyo bila kulipa kodi huku mara kwa mara akimtuhumu kuwa yeye ni mchawi.
Uchawi (1)-001 
Georgina, maarufu kwa jina la Mama Irene alisema kuwa, ilifika hatua mpangaji huyo akawa anamtukuna hadharani, yeye na mwanaye Irene huku akisambaza maneno kuwa ni mchawi.
“Nakumbuka ilikuwa Agosti 31 (mwaka huu), mpangaji huyo alianza kumtukana mwanangu akidai kuwa tumechukua nguo zake na kuzikata kila moja kwenye pindo, jambo lililonifanya nimfuate kumuuliza, lakini nilipomsogelea tu mume wangu akaja na kuanza kumpiga Irene akidai ni kweli tulifanya hivyo.
“Baada ya tukio hilo, mume wangu akawa hanisemeshi, hatoi fedha ya matumizi na wala halali chumbani kwangu. Akawa anakula kwa mpangaji huyo kisha analala chumba cha wageni.
Uchawi (3)-001
Mjumbe wa nyumba kumi, Kuruthumu Bakari.
“Nilitoa taarifa kwa mjumbe wa nyumba kumi (Kuruthumu Bakari) lakini aliniambia nilipeleke shauri langu kwenye Baraza la serikali za mitaa,” alisema mama mwenye nyumba.
Kwa upande wake Mama Alex alikanusha madai ya kuishi bila kulipa kodi (japo hana mkataba) pamoja na kuchepuka na mume wa Georgina, akaongeza kuwa kinachomsumbua mahali hapo ni vitendo vya kichawi anavyokuwa anafanyiwa, kikiwemo hicho cha kanga zake kukatwa vipande kwenye pindo.
Alipoulizwa kwa nini asihame, mama Alex alifunguka: “Siwezi kuhama kwa sababu sina tatizo na baba mwenye nyumba, nitatoka fedha yangu itakapoisha.”
Baadhi ya majirani wa Georgina walisema kuwa, Mama Alex ni mshari na amekuwa akitifuana na mama mwenye nyumba mara kwa mara.
Juhudi za kumtafuta baba mwenye nyumba na mume wa mpangaji huyo kuzungumzia jambo hilo hazikuzaa matunda.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.