Wednesday, September 23, 2015

Anonymous

JUX: Jackie Cliff Anajua Nipo na VANESSA Mdee!

Jux amedai kuwa Jackie Cliff (aliyekuwa girlfriend wake) aliyedaiwa kukamatwa na madawa ya kulevya nchini China na kufungwa jela, anaendelea vizuri na anafuatilia kila kitu kinachoendelea Bongo.
jux na Jackie
Jux amesema Jackie anajua mahusiano yake na Vanessa Mdee.
“Yeah tunawasiliana tunaongea,” amesema Jux. “Anajua kila kitu kinachoendelea. Tunaongea vizuri, yuko poa kabisa na habari za Bongo kila kitu anajua yaani,” Jux alikiambia kipindi cha Planet Bongo cha East Africa TV.
“Kuna habari nyingine hata mimi nashangaa anajuaje, kwa sababu kuna rafiki zake wengine wanaenda kumuona, pia mimi ni kijana I want to move on in my life, na yeye mwenyewe anajua inabidi niendelee na maisha, kikubwa zaidi tunawasiliana na hatuna mahusiano yoyote mabaya.”

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.