Nahodha wa Taifa Stars, Nadir Haroub ‘Cannavaro’.
Mohammed Mdose, Dar es Salaam
NAHODHA wa Taifa Stars, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, amesema kuwa kama washambuliaji wa Stars wangekuwa makini basi wangeweza kuwafunga Nigeria lakini kocha wao Charles Boniface Mkwasa, amesema hali hiyo ni ya kawaida.
NAHODHA wa Taifa Stars, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, amesema kuwa kama washambuliaji wa Stars wangekuwa makini basi wangeweza kuwafunga Nigeria lakini kocha wao Charles Boniface Mkwasa, amesema hali hiyo ni ya kawaida.
Stars na Nigeria zilikutana juzi Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam, kwenye mchezo wa kufuzu Kombe la Mataifa Afrika (Afcon) 2017
nchini Gabon na kumaliza dakika 90 bila kufungana, licha ya Stars
kuutawala mchezo na kukosa nafasi kadhaa za wazi za kufunga.
Wachezaji wa Stars, Thomas Ulimwengu na Mrisho Ngassa walipata nafasi za kufunga lakini mipira yao haikuwa na macho ya kupenya langoni mwa Nigeria.
Wachezaji wa Stars, Thomas Ulimwengu na Mrisho Ngassa walipata nafasi za kufunga lakini mipira yao haikuwa na macho ya kupenya langoni mwa Nigeria.
Cannavaro alisema Stars ilijitahidi kuikamata Nigeria kila idara na
walikuwa na uwezo wa kuwafanya watakavyo lakini walikwama katika
kukwamisha mipira wavuni.
“Siwezi kumtaja mmojammoja lakini tulichoshindwa ni kufunga mabao lakini tuliwamudu kila idara, kama tungekuwa makini basi tungewafunga, nafasi bado tunayo kujirekebisha katika mechi zijazo,” alisema Cannavaro.
“Siwezi kumtaja mmojammoja lakini tulichoshindwa ni kufunga mabao lakini tuliwamudu kila idara, kama tungekuwa makini basi tungewafunga, nafasi bado tunayo kujirekebisha katika mechi zijazo,” alisema Cannavaro.
Kwa upande wa Mkwasa, alisema kuwa kukosa mabao ya wazi kama
walivyofanya washambuliaji wake ni tatizo kubwa lakini akagoma kutupa
lawama kwa mchezaji yeyote, badala yake akasisitiza atafanya kila
awezalo kulimaliza tatizo hilo.
“Siyo muda wa kuanza kumlaumu mmojammoja ila cha kufanya ni kulifanyia kazi tatizo kuona hatufanyi tena kosa hili ambalo limetugharimu kwenye mchezo ambao tulikuwa na uwezo wa kushinda,” alisema Mkwasa.
“Siyo muda wa kuanza kumlaumu mmojammoja ila cha kufanya ni kulifanyia kazi tatizo kuona hatufanyi tena kosa hili ambalo limetugharimu kwenye mchezo ambao tulikuwa na uwezo wa kushinda,” alisema Mkwasa.

Note: Only a member of this blog may post a comment.