Friday, August 28, 2015

Anonymous

Christian BELLA anataka mwanae acheze soka la kulipwa Ulaya!

Christian Bella amesema anajipanga kumpeleka mtoto wake wa kiume kwenye shule za mpira nchini Sweden.
11335818_1114629311898044_1443085020_n Bella akiwa na mwanae pamoja na mke wake
Bella ameiambia Bongo5 kuwa anajisikia fahari kumchagulia mwanae kwenda kwenye shule za mpira kwa kudai mchezo huo unalipa sana kwa nchi za Ulaya. 

“Unajua mzazi ndio mtu pekee anayeweza kumpeleka mtoto wake sehemu salama,” amesema muimbaji huyo. “Ndio maana mimi nikaona nikimpeleka mwanangu kwenye shule za kucheza mpira nitakuwa nimemsaidia sana. Mpira unalipa sana Ulaya.”
“Unajua baba yake ni mwanamuziki na naamini pale alipo ndani yake ana chembechembe za muziki, lakini nikaona tu nimtafutie kitu kingine ambacho pia kinaweza kuwa bora,” aliongeza.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.