STEVE NYERERE (KINONDONI)
Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ ni msanii aliyejinyakulia umaarufu kwa kuigiza sauti ya Mwalimu Nyerere na hata viongozi wengine akiwemo Rais Kikwete. Hivi karibuni msanii huyo ameweka wazi nia yake ya kulinyakua jimbo la Kinondoni kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwa tayari kupambana na mwakilishi wa jimbo hilo kwa sasa kupitia chama hicho, Mhe. Idd Azzan.
KING MAJUTO (TANGA MJINI)
Jina lake siyo geni kwenye anga la sanaa kipengele cha uchekeshaji. Jina lake halisi anaitwa Amri Athumani. Amekwisha tangaza nia ya kuliwania Jimbo la Tanga Mjini kupitia CCM, huku akitajwa kuwa mwiba mkali kwa mbunge wa sasa kupitia chama hicho, Mhe. Omari Nundu.
Awali, alitangaza kulitaka jimbo hilo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), lakini kwa sasa amebadili upepo na tayari ameonesha nia kulitaka Jimbo la Morogoro mjini kupitia chama kipya cha ACT-Wazalendo na kwamba kwa sasa ni kada aliye hai wa chama hicho, ingawa duru za siasa hazimuoneshi kuwa na upinzani mkubwa kwa mbunge wa sasa kupitia CCM, Mhe. Aziz Aboud.
JIMY MAFUFU (MBEYA MJINI)
Filamu za Uliyemchokoza Kaja na Ndondo ndizo zilimpa jina kubwa kwenye ulimwengu wa sanaa ya uigizaji, ingawa ni msanii wa muda mrefu! Amejipambanua kuwa kada hai wa CCM na kesho (Ijumaa) ataelekea Mbeya mjini tayari kupambana na mbunge wa sasa wa jimbo hilo kupitia Chadema, Mhe. Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na kwamba amejiapiza kulitwaa.
PROF. JAY (MIKUMI)
Joseph Haule ‘Prof. Jay’ ndiye alikuwa wa kwanza kabisa kuonesha shauku ya kujitosa kwenye ulingo wa siasa na tayari alishatangaza nia ya kuliwania Jimbo la Mikumi huku akijivunia chimbuko la babu yake na kwamba amejiandaa kwa sera thabiti zitakazo mhakikishia ushindi kupitia Chadema dhidi ya mwakilishi wa jimbo hilo kwa sasa kupitia CCM, Mhe. Abdulsalaam Seleman Amer.

Note: Only a member of this blog may post a comment.