Sunday, March 13, 2016

Anonymous

HAYA NDIO MAISHA: Mastaa Jason, Daphne Wajiachia Ufukweni [+PICHAZ]

jason 
Staa wa muziki wa R&B, Jason Derulo na mpenzi wake, Daphne Joy wakiwa ufukweni.
CASA ARAMARA, Mexico
ANAPIGA kote kote! Staa wa muziki wa R&B, Jason Derulo na mpenzi wake, Daphne Joy wameonyesha kuwa wanapendana sana baada ya kuonekana wakijiachia vya kutosha huko Punta Mita, Mexico, Jumanne ya wiki hii.
Jason Derulo ambaye amewahi kutoka na msanii mwenzake, Jordin Spark aliyedumu naye kwa miaka mitatu, sasa ameangukia kwenye penzi la mrembo Daphne Joy ambaye ni ‘ex’ wa staa wa hip hop, 50 Cent aliyezaa naye mtoto mmoja, Sire Jackson, 3.
3209B77600000578-3484448-image-a-20_1457548505194Wakifurahia jambo.
Staa huyo mwenye miaka 26 ambaye kwa sasa anatisha na Ngoma ya Hello Friday na mpenzi wake huyo aliyenaye kwa miezi minne sasa walipata nafasi ya kujiachia vilivyo kwenye Fukwe za Casa Aramara huku wakionyesha mapenzi ya hadharani na watu kuwashangaa.
Wakiwa huko walicheza michezo mbalimbali kama kukimbizana, kumwagiana maji, kuendesha pikipiki zinazojulikana kama ATV pamoja na mingine mingi.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.