Muimbaji mrembo wa nchini Kenya, Avril huenda akarekodi wimbo na muimbaji wa nyimbo za injili, Christina Shusho siku za usoni.
Hata hivyo amedai kuwa kurekodi wimbo na msanii huyo wa Tanzania hakumaanishi kuwa anaingia kwenye muziki wa injili.
Avril alikutana na Christina Shusho wiki iliyopita kwenye hafla ya
Catholic University Dreamz Come True Initiative jijini Nairobi
ambapo Shusho alimuita jukwaani alipokuwa akihudumu na kumuombea pamoja na wachungaji wengine.
ambapo Shusho alimuita jukwaani alipokuwa akihudumu na kumuombea pamoja na wachungaji wengine.
“That awesome moment when Christina Shusho calls you on stage and the
Pastors in the house come to pray for you…too awesome ,” aliandika
Avril kwenye picha aliyoweka Instagram.
Wakiwa jukwaani wawili hao walizungumza kuhusu kufanya kazi pamoja siku za usoni.

Note: Only a member of this blog may post a comment.