Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeendelea na zoezi la kuwaapisha wabunge wateule mbele ya Spika Job Ndugai.
Kiapo cha wabunge hao ni ishara ya kupokea na kuanza majukumu yao ya kuwawakilisha wananchi.
Hiki ni kikao cha pili cha Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Zoezi la kuapishwa wabunge wateule limeanza majira ya saa tatu asubuhi baada ya kuahirishwa jana.
Baadhi ya wabunge waliopata nafasi ya kuapishwa asubuhi ya leo wamekula kiapo cha utii na uaminifu kuonyesha utayari wa kuwatumikia wananchi.
Bunge limeahirishwa saa tano kamili asubuhi hadi saa 11 jioni ambapo linaendelea na zoezi la kuwaapisha wabunge wateule waliobaki.
Kiapo cha wabunge hao ni ishara ya kupokea na kuanza majukumu yao ya kuwawakilisha wananchi.
Hiki ni kikao cha pili cha Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Zoezi la kuapishwa wabunge wateule limeanza majira ya saa tatu asubuhi baada ya kuahirishwa jana.
Baadhi ya wabunge waliopata nafasi ya kuapishwa asubuhi ya leo wamekula kiapo cha utii na uaminifu kuonyesha utayari wa kuwatumikia wananchi.
Bunge limeahirishwa saa tano kamili asubuhi hadi saa 11 jioni ambapo linaendelea na zoezi la kuwaapisha wabunge wateule waliobaki.

Note: Only a member of this blog may post a comment.