Rais John Pombe Magufuli amemteua mheshimiwa KASSIM MAJALIWA pichani juu ambaye ni mbunge wa Ruangwa kuwa Waziri mkuu wa Tanzania. Hivi punde asubuhi hii jina lake limetangazwa rasmi bungeni Dodoma na kinachosubiriwa muda huu ni jina hilo kupigiwa kura ambapo wabunge wametoka mapumziko ya muda mfupi kusubiri karatasi za kupigia kura ziandaliwe na pia wasifu wa Waziri mkuu uandaliwe ili usomwe na mwanasheria mkuu kwa kufuata itifaki.Endelea kufuatilia zaidi hapa hapa kandiliyetu.com


Note: Only a member of this blog may post a comment.