Manispaa ya Kinondoni jana ilisababisha vilio kwa wakazi wa maeneo wa wilaya hiyo ilipoanza ubomoaji wa nyumba zilizojengwa maeneo ya wazi na hifadhi kinyume cha sheria
Juzi, Kamishna wa Ardhi wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk Moses Kusirika alitangaza operesheni ya kubomoa nyumba hizo kuanzia jana na kuwa baada ya Kinondoni watahamia wilaya nyingine na mikoani pia.
Miongoni mwa maeneo yaliyokumbwa na bomoabomoa hiyo jana ni Mwenge, Sinza, Biafra-Bwawani na Mivumoni.
Ubomoaji katika mtaa wa TRA Mwenge, ulianza saa 10 alfajiri, ambapo nyumba za biashara na makazi 15 zilibomolewa chini ya ulinzi mkali wa polisi.
Huku baadhi wakiangua vilio, wakazi waliokumbwa na hatua hiyo walilalamika wakidai hawakuwa na taarifa za kuwapo kwa ubomoaji huo, jambo lililosababisha baadhi yao kushindwa kuokoa mali zilizokuwa ndani.
Note: Only a member of this blog may post a comment.