Mshambuliaji wa klabu ya Chelsea, Diego Costa ameachwa katika kikosi
cha timu ya taifa ya Hispania katika michezo miwili ya wiki ijayo. Kocha
Vicent Del Bosque amesema hajafurahishwa na tabia ya mchezaji huyo
aliyoifanya dhidi ya Arsenal.
Hispania inahitaji point moja tu ili kufuzu katika michuano ya
mataifa ya Ulaya na wiki ijayo itapambana na Luxembourg na Ukraine
katika michezo yake ya mwisho ya kundi.
Mshambuliaji wa Juventus ambaye anafanya vizuri kwa sasa, Alvaro
Morata ameitwa kikosini na anatarajiwa kushika nafasi ya Diego Costa
katika kikosi cha kwanza.
Wachezaji wenza watatu wa Chelsea Cesar Azzpilicueta, Cesc Fabregas
na Pedro Rodriguez wote wameitwa sambamba na Carzola wa Arsenal na
wachezaji wawili wa Manchester United, David De Gea na Juan Mata huku
David Silva wa Manchester City akikamilisha orodha ya wachezaji 23.

Note: Only a member of this blog may post a comment.