Saturday, September 12, 2015

Anonymous

Muigizaji DESMOND Elliot wa Nigeria Asema Anapumzika Kufanya Filamu Kutokana na Majukumu ya Ubunge!

Muigizaji maarufu wa Nollywood ambaye sasa ni Mbunge, Desmond Elliot amesema kuwa kwa sasa anapumzika kufanya filamu ili ajikite vema kwenye siasa.
Amesema kuwa halitakuwa jambo la busara kuchanganya mambo ya uigizaji na maisha yake mapya ya siasa.
“Kazi ya ubunge sio rahisi, nitaonekana sio muwajibikaji kama nitaendelea kuigiza huku nina majukumu mengi ya ubunge” Desmond aliiambia Myjoyonline.
Desmond alijitosa kwenye siasa mwaka 2014 na kugombea Ubunge (Lagos State of Assembly) kwenye uchaguzi wa mwaka 2015, ambapo alishinda kupitia chama chake cha APC.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.