Thursday, September 10, 2015

Anonymous

Mke Wangu Nilimpatia Club, Mazingira Ambayo Wengi Wanadhani Si Mazuri Kwa Mwanamke – MR BLUE

Mr Blue a.k.a byser ametumia wimbo wake mpya kutoa ujumbe kwa mashabiki ambao hawajaoa au kuolewa, kuwa mtu akiamua anauwezo wa kumbadilisha mtu na kumfanya astahili kuwa mke au mme bila kujali aina ya maisha aliyopitia.

Byser amesema kuwa wimbo wake mpya ‘Baki na Mimi’, unagusa moja kwa moja maisha yake na mke wake Warda.
“Wimbo huu unagusa maisha ya mimi na mke wangu Warda kwa asilimia kubwa, wengi hawajui kuwa mke wangu nilikutana naye club, mazingira ambayo wengi wanadhani si mazuri kwa mwanamke, lakini kwangu ni tofauti kwa kuwa mke wangu ana sifa zote za kuwa mke,” alisema Blue.
Mr Blue na mke wake wamepata mtoto wa pili wa kike wiki iliyopita. Wamempa jina la Khairriyah.
Chanzo: Mtanzania

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.