Hiki ni kipindi ambacho wasanii wengi wa Tanzania watanufaika kwa
mashavu mengi kutoka kwa wanasiasa wanaowania nafasi za uongozi kwenye
uchaguzi mkuu ambao kampeni zake zinatarajia kuanza siku nne zijazo.
Kamati za kusajili wasanii watakaotumika kwenye kampeni katika kambi
mbalimbali zinaendelea kukaa kutengeneza vikosi japo tayari baadhi ya
wasanii wanajulikana watakuwa upande upi.
Hata hivyo muigizaji wa filamu, Vincent Kigosi maarufu kama Ray ana mtazamo tofauti. Hiki ndicho alichoandika kwenye Instagram:
Usiku wa jana nimetafakari vi2 vingi sana kuhusu Nchi yangu
iliyobarikiwa kila aina ya utajiri wa madini mbuga za wanyama wakiwemo
aina mbalimbali za wanyama wa kuvutia na hekta kubwa za misitu Ila
ninaona vipofu wengi sana wasiolewa nini 2lichobarikiwa ndani ya
Tanzania ye2. 2meingizwa mikenge mingi sana katika mikataba tena mibovu
bajeti kandamizi Kwa wa2 wa hali ya chini mifumuko ya bei kila kukicha
hali ngumu kwa wasanii wa Tanzania kila siku ahadi zisizotekelekeza why
nasema hivyo wasanii wenzangu?
2meumia kwa kipindi kirefu sana bila msaada wowote ha2na haki miliki
wa kazi ze2, zinaibiwa kama njugu sokoni kariakoo yani 2li2pwa kama taka
taka kwenye dampo lakini sasa hivi kipindi cha uchaguzi ndio 2naonekana
umuhimu we2 tuamke kuwaambia wananchi wachague viongozi makini
watakaoweza ku2vusha Watanzania kwenda ha2a nyingine.
Tuna wa2 wengi sana nyuma ye2 wanaotuamini sisi wasanii kama kioo cha jamii tusiwapoteze Watanzania kuwaambia Viongozi wa chama flani ndio wanafaa kwa vijisenti vidogo 2navyopewa. Watanzania huu ni wakati sahihi waku2lia na kuwachagua viongozi makini wanaofaa Ni katika kukumbushana 2 waswahili wanasemaje utakaokatanao kuni ndio utakaota nao moto.
Tuna wa2 wengi sana nyuma ye2 wanaotuamini sisi wasanii kama kioo cha jamii tusiwapoteze Watanzania kuwaambia Viongozi wa chama flani ndio wanafaa kwa vijisenti vidogo 2navyopewa. Watanzania huu ni wakati sahihi waku2lia na kuwachagua viongozi makini wanaofaa Ni katika kukumbushana 2 waswahili wanasemaje utakaokatanao kuni ndio utakaota nao moto.

Note: Only a member of this blog may post a comment.