Klabu ya soka ya Simba
bado inaendeleza usajili wake kimya kimya kwani baada ya kusajili
wachezaji kadhaa katika msimu huu bado huenda ikamuongeza mshambuliaji
wa kimataifa wa Senegal aliyekuwa anaichezea klabu ya CF Mounana ya Gabon Papa Niang.
Simba bado hawajathibitisha usajili huo kwani inaripotiwa atatua Dar Es Salaam ndani ya siku mbili hizi, uvumi wa mshambuliaji huyo kujIunga na Simba unatiwa nguvu kwa mchezaji huyo kuwa huru hadi hivi sasa hivyo huenda Simba ikatumia nafasi hiyo kumnasa.
Papa Niang aliyezaliwa December 5 1988 Matam Senegal amewahi kuchezea vilabu vya Vostok Oskemen ya Kazakhstan, Al-Shabab Sports Club ya Kuwait na kuichezea klabu ya CF Mounana ya Gabon aliyoichezea kwa takribani mwaka mmoja.
Licha ya dirisha la usajili kufungwa saa 6 usiku August 20 uwezekano wa Simba
kumnasa staa huyo upo kwani baada ya kufungwa kwa dirisha la usajili
usiku wa August 20 timu zinaruhusiwa kusajili ila kwa malipo ya Tsh
500,000/= kwa kila mchezaji itakao muongeza kikosini kabla ya msimu wa
Ligi haujaanza.
CHANZO CHA HII STORI: SALEH JEMBE

Note: Only a member of this blog may post a comment.