Monday, August 3, 2015

Anonymous

MGOMBEA URAIS WA CHAUMMA ACHUKUA FOMU!

Ofisa wa NEC, Adam Nyando (kushoto) akimkabidhi fomu ya urais, Hashim Rungwe.
Ofisa wa NEC, Crecencia Mayalla (kushoto), akimpatia maelekezo mgombea namna ya kujisajili katika daftari la wagombea.
Hashim Rungwe (kushoto) akiwa na mgombea mwenza, Isa Abbas Husein (kulia), wakati wakipewa maelekezo ndani ya ofisi hizo.1.Mgombea urais, Hashim Rungwe kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma) akiwaonyesha wanahabari (hawapo pichani) mkoba ulio na fomu ya kugombea urais.
Hashim Rungwe (kulia) akiwa na mgombea mwenza, Isa Abbas Husein (kushoto), wakitoka ndani ya ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).Wanahabari wakiwa nje ya ofisi za NEC wakimsubiri mgombea urais wa Chaumma.
Gari la Chaumma likiwa nje ya ofisi za NEC.
CHAMA cha Ukombozi wa  Umma (CHAUMMA) kupitia mgombea wake, Hashim Rungwe Spunda pamoja na mgombea mwenza, Issa Abbas Husein hii leo wamechukua fomu ya kupeperusha nafasi ya Urais kupitia chama chao. 

Mgombea huyo  amechukua fomu hiyo  mapema hii leo katika makao makuu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi jijini Dar es Salaam,  ambapo aliambatana na mgombea mwenza kupitia chama hicho kwa ajili ya kuchukua fomu. 

Aidha katika maelekezo ya fomu hiyo inamtaka mgombea kuzunguka mikoa yote ya Tanzania na Zanzibar kusaka wadhamini 200 na hivyo kufikia Agosti 21 fomu hiyo kurudishwa katika ofisi za tume.
(NA DENIS MTIMA/GPL)

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.