Friday, June 12, 2015

Anonymous

Unajua sababu iliyofanya Afande Sele akafukuzwa Jeshi? Kipaji cha Langa kiligundulika lini?…#255 (Audio)

Kesho ni June 13.. ni siku ya Kumbukumbu ambayo alifariki mmoja wa rappers wakali waliowahi kutokea TZ, Langa ambae alifariki June 13 2013.. leo anasikika Mama mzazi wa msanii huyo ambaye amesema aligundua kipaji cha mwanae tangu akiwa na umri wa mwaka mmoja wakiwa Kigoma, alikuwa anapenda kucheza na kuimba pekeyake. 

Afande Sele, ni mmoja ya mastaa wa Bongo Fleva ambao waliwahi kupitia Jeshini, jamaa alifukuzwa kwa kesi ya utovu wa nidhamu, unajua nini kilifanya akafukuzwa? 

Afande Sele amesema alitimuliwa jeshini Chukwani Zanzibar baada ya kukutwa kwenye maeneo wanayokaa askari wa kike, wakapelekwa kwenye makao makuu ya Jeshi alafu baadae wakasimamishwa. 

Msanii JI aliwahi kuhit na wimbo wa kidato kimoja, leo kasikika akisimulia safari yake mpaka kuingia kwenye muziki.. kumbe jamaa aliwahi kuwa fundi, baadae akapitia mpaka kumiliki saluni.. mwisho wake akaingia kwenye usanii wa muziki.

Sauti ya 255 iko hapa, ukibonyeza play hapa chini utazisikia stori zote....

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.