Tuesday, June 23, 2015

Anonymous

SIMBA SC Hii Utailewa Tu!

Rais wa Simba, Evans Aveva alitumia dakika 17 kutangaza mabadiliko ya benchi la ufundi la timu hiyo litakalokuwa chini ya kocha Muingereza Dylan Kerr. 

Kerr ambaye ni beki wa zamani mwenye miaka 48, alikuwa na mafanikio makubwa kama mchezaji kabla ya kugeukia ukocha.
Katika miaka tisa ya uchezaji soka, Kerr amecheza Ligi Kuu England akiwa na klabu za Leeds United na Reading FC, pamoja na Arcadia Shepherds FC ya Afrika Kusini mwishoni mwa miaka1980.

Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa kocha Kerr ataigharimu Simba kiasi cha dola 9,000 ( Sh20 milioni) kila mwezi, kwani katika fedha hizo kocha huyo atakuwa akipokea kiasi cha dola 6,000 (Sh 13.2milioni ) kwa mwezi huku kiasi kinachobaki kitatumika kumlipia gharama mbalimbali za nyumba na usafiri.

Akitangaza mabadiliko hayo, Aveva alisema kocha Kerr atawasili nchini mwishoni mwa wiki tayari kuchukua nafasi ya Mserbia Goran Kopunovic.

Aveva alisema Kerr atasaini mkataba wa mwaka mmoja, pia kutakuwa na uwezekano wa kuongezewa mwingine endapo atafanya vizuri licha ya kuwa hana uzoefu wa kufundisha soka Afrika Mashariki, lakini amewahi kufanya kazi nchini Afrika Kusini.
“Tulikuwa na makocha kama watano ambao tulikuwa tunawaangalia katika kumpata mmoja, hata huyo Kim (Poulsen) alikuwapo ingawa siyo kama ambavyo inatamkwa ila baadaye tukaamua tumpe nafasi Kerr,” Aveva. 

“Tunaamini Kerr ataisaidia Simba kupata mabadiliko makubwa katika Ligi Kuu, kazi yetu kama uongozi ni kumuandalia mazingira mazuri ya kufanya kazi akiwa na wasaidizi wake,”.

Kerr kabla ya kutua Simba aliwahi kufundisha klabu ya Hai Phong ya Vietnam pamoja na Mpumalanga Black Aces ya Afrika Kusini huku akitumia muda mwingi kuwa kocha msaidizi katika klabu mbalimbali.
Kerr atakuwa akisaidiwa na Seleman Matola pamoja na kocha mpya wa makipa Mkenya Abdul Idd Salim.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.