Wednesday, January 11, 2017

Unknown

Mbwana Samatta Aletewa Changamoto Mpya na Timu Yake ya KRC Genk

Siku 14 zimepita toka mshambuliaji wa KRC Genk Nikolaos Karelis ambaye alikuwa anashindania namba na mtanzania Mbwana Samatta atangazwe kuwa atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha miezi 8 hadi 9 kufuatia jeraha la goti la kushoto alilolipata wakati wa mchezo dhidi ya KAA Gent dakika ya 51 December 27. 
Karelis 
January 10 2017 KRC Genk imetangaza kukamilisha usajili wa mshambuliaji Jose Naranjo kutokea Celta Vigo ya Hispania, hiyo itakuwa ni changamoto mpya kwa Mbwana Samatta kuendelea kupambania namba ya kucheza na Naranjo katika kipindi ambacho Karelis atakuwa nje. 
Jose Naranjo 
Jose Naranjo amejiunga na KRC Genk ya Ubelgiji akitokea Celta Vigo ya Hispania kwa mkataba wa miaka mitatu na nusu, Naranjo mwenye umri wa miaka 22 amewahi kuichezea Villarreal kwa mkopo mwaka 2014 akitokea Recreativo.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.