Monday, June 15, 2015

Anonymous

RATIBA ya kuaga mwili wa Marehemu Shehe Mkuu TZ, Mufti Shaaban Simba pamoja na mazishi imetolewa… (Audio)

Stori ya Msiba wa aliyekuwa Sheikh Mkuu Tanzania, Mufti Sheikh Issa Shaaban Bin Simba imechukua nafasi kubwa sana kwa kuripotiwa kwenye vyombo vingi vya Habari. 

Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhadi Mussa Salum nimemnukuu akithibitisha juu ya msiba huo >>> “Ni kweli Mheshimiwa Mufti amefariki.. Kesho saa nne asubuhi Waislamu na Viongozi wote watajumuika Makao Makuu ya BAKWATA, Kinondoni Muslim kuuaga mwili wa Sheikh. Mchana mwili wa Sheikh utasafirishwa kwenda Shinyanga, atazikwa siku ya Alhamisi“>>>– Sheikh Alhadi Mussa Salum  

Hapa anamzungumzia Marehemu Mufti Simba>>> “Mufti alikuwa  na sifa ya kuwa Kiongozi wa Waislamu. Alikuwa mvumilivu sana na msamehevu katika Utawala wake. Angekuwa hana subira Waislamu wasingekuwa na uvumilivu“>>>– Sheikh Alhadi Mussa Salum.
Bonyeza play hapa chini kusikiliza live...

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.