Heka heka ya
leo inatoka maeneo ya Ilala, Dar es salaam, inahusu mama wa bibi harusi
kulazimisha maharusi wakapime kwanza kabla ya kuondoka kwenda kuishi
pamoja.
Kitendo cha mama wa bibi harusi na
shangazi kulazimisha maharusi hao kwenda kupima kwa kulala mbele ya gari
makusudi ili lisiondoke lilisababisha mvutano mkubwa miongoni mwa ndugu
wa pande zote mbili ambao hawakuweza kufikia muafaka.
Baada ya mvutano mkubwa awali bwana harusi alikubali kwenda hadi Hospitali ya Amana
kupima akiongozana na bibi harusi pamoja na ndugu wa pande zote mbili
lakini walipofika gafla alikataa kupima kwa madai amedhalilishwa na
kutaka arudishiwe fedha zake.
Inasemekana kuna mmoja wa watu
aliwadokeza ndugu wa bibi harusi kuwa bwana harusi ni mgonjwa ingawa bw
ana harusi amekiri tayari alishatembea na mke wake muda mrefu.
Isikilize hekaheka yote hapa chini...

Note: Only a member of this blog may post a comment.