HABARI PICHAZ: LOWASSA HAKAMATIKI!
Waziri
Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania kupitia
tiketi ya CCM, Mh. Edward Lowassa akiwapungia wananchi wa mji wa Mpanda,
Mkoani Katavi waliojitokeza kumlaki, wakati alipofika kwenye Ofisi za
CCM Wilaya ya Mpanda, Mkoani Katavi, alikofika jana Juni 14, 2015 kwa
ajili ya kutafuta udhamini wa wanaCCM ili apate ridhaa ya Chama cha
Mapinduzi (CCM) kuwania Urais wa Tanzania, kwenye Uchachuzi Mkuu,
Unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015. alie mbele yake ni Mwenyekiti wa
CCM Mkoa wa Katavi, Mselem Said Abdallah.
Mh.
Edward Lowassa akipokea fomu zenye majina ya wanaCCM wa Mkoa wa Katavi
Juni 14, 2015, waliomdhani ili apate ridhaa ya Chama cha Mapinduzi
(CCM) kuwania Urais wa Tanzania, kwenye Uchachuzi Mkuu, Unaotarajiwa
kufanyika Oktoba 25, 2015. Anaekabidhi fomu hizo ni Katibu wa CCM Wilaya
ya Mpanda, Bi. Elizabert Kashira. Mh. Lowassa amepata udhamini wa
wanaCCM 3440 mkoani Katavi.
Mwenyekiti
wa CCM Mkoa wa Katavi, Mselem Said Abdallah akizungumza machache mara
baada ya Mh. Lowassa (pili kulia) kukabidhiwa fomu za wadhamini wa CCM
za kumuwezesha kutata ridhaa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwania Urais
wa Tanzania, kwenye Uchachuzi Mkuu, Unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25,
2015. Wengine pichani toka kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa
Shinyanga, Hamis Mngeja, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kigoma, Dkt. Aman
Kaburou pamoja na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mpanda, Beda Katani.

Mwenyekiti
wa CCM Mkoa wa Katavi, Mselem Said Abdallah akimkaribisha Waziri Mkuu
Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania kupitia tiketi ya
CCM, Mh. Edward Lowassa ili aweze kuwashukuru wanaCCM wa Mpanda kwa
kumdhani ili apate ridhaa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwania Urais wa
Tanzania, kwenye Uchachuzi Mkuu, unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25, 2015.

Waziri
Mkuu Mstaafu na Mtangaza nia ya kuwania Urais wa Tanzania kupitia
tiketi ya CCM, Mh. Edward Lowassa akiwapungia mkomo maelfu ya wanaCCM
pamoja na wananchi wa Mji wa Mpanda, waliofurika kwenye ofisi za CCM
Wilaya ya Mpanda, Mkoani Katavi Juni 14, 2015.Mh. Lowassa amepata
udhamini wa wanaCCM 3440 mkoani Katavi.
USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK
TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)
Note: Only a member of this blog may post a comment.