Monday, June 15, 2015

Anonymous

Mheshimiwa SITTA Wa Kwanza Kurudisha Fomu Ya Urais CCM

Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta jana alikamilisha mchakato wa kusaka wadhamini wa maombi yake ya kuwania urais kupitia CCM na leo anatarajia kuwa wa kwanza kurejesha fomu hizo makao makuu ya chama hicho mjini Dodoma. 

Sitta ambaye ni miongoni mwa wanaCCM 32 waliokwishachukua fomu kuwania nafasi hiyo, atarejesha fomu hizo baada ya kupata saini za wanaCCM katika mikoa 21 nchini. Kila mgombea anatakiwa kupata wadhamini 450 katika mikoa 15, kati ya hiyo mitatu ya Zanzibar. 

Akizungumza na wakazi wa Itundu na mjini Urambo alikomalizia mzunguko huo, Sitta alisema kazi ya urais si lelemama ila ataimudu kwani anaifahamu vizuri nchi. 

Alisema endapo atateuliwa na chama chake kugombea urais na kushinda ataimarisha Muungano na kupambana na ufisadi na uonevu kwa wananchi ili kila mtu afurahie maisha yake.
Aliahidi kuiimarisha CCM kiuchumi ili isiyumbishwe na matajiri.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.