Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta
jana alikamilisha mchakato wa kusaka wadhamini wa maombi yake ya
kuwania urais kupitia CCM na leo anatarajia kuwa wa kwanza kurejesha
fomu hizo makao makuu ya chama hicho mjini Dodoma.
Sitta ambaye ni miongoni mwa wanaCCM 32
waliokwishachukua fomu kuwania nafasi hiyo, atarejesha fomu hizo baada
ya kupata saini za wanaCCM katika mikoa 21 nchini. Kila mgombea
anatakiwa kupata wadhamini 450 katika mikoa 15, kati ya hiyo mitatu ya
Zanzibar.
Akizungumza na wakazi wa Itundu na mjini
Urambo alikomalizia mzunguko huo, Sitta alisema kazi ya urais si
lelemama ila ataimudu kwani anaifahamu vizuri nchi.
Alisema endapo atateuliwa na chama chake
kugombea urais na kushinda ataimarisha Muungano na kupambana na ufisadi
na uonevu kwa wananchi ili kila mtu afurahie maisha yake.
Aliahidi kuiimarisha CCM kiuchumi ili isiyumbishwe na matajiri.


Note: Only a member of this blog may post a comment.