Monday, April 27, 2015

Anonymous

EDEN HAZARD: "Sijui kama nastahili kushinda hii tuzo, lakini ni vizuri kwangu"

Eden Hazard wa Chelsea ameshinda tuzo ya PFA ya mchezaji bora wa mwaka.
Nyota huyu raia wa Ubelgiji ameifungia Chelsea magoli 18 katika mashindano yote msimu huu na amekuwa na mchangu kubwa kwa The Blues kutwaa kombe la ligi kuu kwa mara ya kwanza kutoka mwaka 2010.


Chelsea ikishinda mechi mbili zijazo dhidi ya Leicester na mechi ya nyumbani dhidi ya Crystal Palace wanaweza kuwa mabingwa.
Baada ya kufanikiwa kupata tuzo hiyo, Hazard amesema: "Nina furaha sana. siku moja nahitaji kuwa bora na nilichokifanya msimu huu ni kucheza vizuri, Chelsea imecheza vizuri".

"Sijui kama nastahili kushinda, lakini ni vizuri kwangu".
"Ni jambo zuri kupigiwa kura na wachezaji-wanajua kila kitu kuhusu mpira wa miguu. Hii ni nzuri. Nina furaha sana".
Wakati huo huo, Harry Kane wa Tottenham Hotspur ameshinda tuzo ya mchezaji bora chipukizi.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.