Ustadhi Swamadu Ramadhan Samata.
Stori: Makongoro Oging’, UWAZI
DAR ES SALAAM: Mwalimu Mkuu wa Chuo cha Madrasa ya Vingunguti, Wilaya ya Ilala jijini Dar, Swamadu Ramadhan Samata anashikiliwa na Jeshi la Polisi Buguruni kwa mahojiano kuhusu upotevu wa mwanandoa Yassin Salum, 30, (pichani).
DAR ES SALAAM: Mwalimu Mkuu wa Chuo cha Madrasa ya Vingunguti, Wilaya ya Ilala jijini Dar, Swamadu Ramadhan Samata anashikiliwa na Jeshi la Polisi Buguruni kwa mahojiano kuhusu upotevu wa mwanandoa Yassin Salum, 30, (pichani).
Taarifa zilizopatikana wiki iliyopita kwa baadhi ya polisi wa kituo
hicho zilisema, Ustadhi Ramadhan anashikiliwa kwa uchunguzi wa madai
kuwa, yeye ndiye aliyeonekana naye mara ya mwisho
Mdogo wa Yasin, Halsa aliliambia gazeti hili kuwa kaka yao ambaye ni
mwalimu wa madrasa na Ustadhi mwalimu mkuu, alitoweka Machi 21, mwaka
huu saa mbili usiku.
“Nakumbuka siku hiyo akiwa na wenzake, walipofika Vingunguti walikaa
nje ya madrasa ambapo Ustadhi anadaiwa kumtumia ujumbe kwamba afanye
hima waonane usiku huo.
“Kaka alijiuliza kwa nini leo ustadhi ananitumia ujumbe mwingi, kuna nini? Ilipofika saa mbili aliwaaga wenzake na kwenda kumuona Ustadhi na tangu hapo hajaonekana, akipigiwa simu haipatikani.
“Tulimfuata chuoni tukakuta milango imefungwa, walioulizwa walisema alikuwa na Ustadhi. Ilipofika saa sita usiku ilibidi familia na wanafunzi wa chuoni kukutana.
“Wengine walikwenda hospitali mbalimbali na vituo vya polisi kikiwepo Kituo cha Polisi Stakishari na kufunguliwa jalada namba STK/RB/464/2016 na jalada Namba VING/PE/04/2016 la Vingunguti, kesho yake saa 12.30 asubuhi Ustadhi alifika chuoni, tulipomuuliza alisema atarudi, kila tukimuuliza anajibu hivyo.
“Hata hivyo, watu wana wasiwasi na Ustadhi, ikabidi itolewe taarifa polisi ambapo alikamatwa,” alisema mdogo wa Yasin.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, SACP Lucas Mkondya alipoulizwa na gazeti hili alikiri kukamatwa kwa Ustadhi Ramadhan.
“Tukio hilo lipo na polisi inaendelea na uchunguzi wakati huo ustadhi huyo tunamshikilia kwa mahojiano,” alisema.
“Tulimfuata chuoni tukakuta milango imefungwa, walioulizwa walisema alikuwa na Ustadhi. Ilipofika saa sita usiku ilibidi familia na wanafunzi wa chuoni kukutana.
“Wengine walikwenda hospitali mbalimbali na vituo vya polisi kikiwepo Kituo cha Polisi Stakishari na kufunguliwa jalada namba STK/RB/464/2016 na jalada Namba VING/PE/04/2016 la Vingunguti, kesho yake saa 12.30 asubuhi Ustadhi alifika chuoni, tulipomuuliza alisema atarudi, kila tukimuuliza anajibu hivyo.
“Hata hivyo, watu wana wasiwasi na Ustadhi, ikabidi itolewe taarifa polisi ambapo alikamatwa,” alisema mdogo wa Yasin.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, SACP Lucas Mkondya alipoulizwa na gazeti hili alikiri kukamatwa kwa Ustadhi Ramadhan.
“Tukio hilo lipo na polisi inaendelea na uchunguzi wakati huo ustadhi huyo tunamshikilia kwa mahojiano,” alisema.

Note: Only a member of this blog may post a comment.