VIDEO Queen Bongo Fatuma Ayubu
‘Bozi’ amesema huwa anaota kila mara kuwa rais ajaye ni Edward Ngoyai
Lowassa anayegombea urais kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA)
kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Bozi aliliambia Risasi Mchanganyiko kuwa anaamini uchumi wa nchi utabadilika na maendeleo yatapatikana endapo waziri huyo mkuu wa zamani atachukua usukani.
“Siyo tu kwamba nampenda Lowassa, bali
hii inatokana na ndoto ninazokuwa naota kila mara kuwa yeye ndiye
atakayekuja kuiongoza nchi yetu baada ya uchaguzi mkuu kufanyika, na
nina imani hata uchumi wa nchi utabadilika,” alisema Bozi.

Note: Only a member of this blog may post a comment.