Boniphace Ngumije na Gladness Mallya, RISASI Mchanganyiko
DAR ES SALAAM: Kuna neno moja tu
linaloweza kusemwa kwa sasa, kuwa tumekwisha, baada ya kubainika kuwa
poda iliyotumika kwa miaka mingi nchini, ambayo ni maarufu kama
Johnson’s Baby Powder inadaiwa kusababisha kansa ya kizazi inayoleta
maafa ikiwemo vifo, Risasi Mchanganyiko lina taarifa kamili.
Taarifa zilizopatikana kupitia mitandao
ya internet, zinadai kwamba kampuni inayotengeneza poda hiyo ya Johnson
and Johnson ya Marekani, Februari 25, mwaka huu ilihukumiwa kulipa faini
ya kiasi cha dola milioni 72 (sawa na shilingi bilioni 144) katika
Mahakama ya Missouri kama fidia kwa mwanamke mmoja aliyefariki dunia kwa
kansa ya kizazi iliyotokana na matumizi ya vipodozi hivyo.
Familia
ya mwanamke huyo, Jacqueline Fox ilitakiwa kulipwa kiasi hicho cha
fedha baada ya mahakama kuridhika kuwa ugonjwa na kifo chake kilitokana
na matumizi ya vipodozi hivyo kwa zaidi ya miaka 35, akitumia poda
pamoja na losheni ya bidhaa hiyo.
Kampuni hiyo ya Johnson & Johnson
ilikabiliwa na tuhuma kwamba kwa miongo mingi, kwa lengo la kufanya
biashara zaidi, haikuwaonya wateja wake kuwa miongoni mwa viungo
vinavyotengeneza bidhaa hiyo, vinasababisha kansa. Zaidi ya kesi 1000
zimefunguliwa huko Missouri na 200 New Jersey, zote zikiilalamikia
bidhaa hiyo.
Fox, aliyeishi Birmingham, Alabama, alisema alitumia Baby Powder na losheni kwa kiwango kikubwa kwa takriban miaka 35, kabla ya kugundulika kuwa na kansa miaka mitatu iliyopita. Alifariki Oktoba mwaka jana akiwa na umri wa miaka 62.
Jere Beasley, ambaye ni wakili wa familia ya Fox, alisema kampuni hiyo ilitambua kuwa inawaongopea wateja wake na mamlaka zinazohusika na vipodozi, wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Msemaji wa kampuni hiyo, Carol Goodrich, alionyesha masikitiko yake kwa hatua hiyo, akisema kwa miaka yote, walitambua kuwa ni jukumu lao kuhakikisha afya na usalama wa walaji wa bidhaa zao.
“Tunaumia pamoja na familia ya mlalamikaji, lakini siku zote tuliamini bidhaa zetu ni bora kutokana na ushahidi wa kisayansi.”
Ushahidi wa kisayansi unaoonyesha kiungo kinachosababisha kansa katika vipodozi hivyo siyo jambo la kificho, kwani kimemo kimojawapo kilichopatikana kutoka kwa mshauri wa kitaalamu aliyeajiriwa na kampuni hiyo kilisema ‘mtu yeyote atakayepinga uhusiano wa matumizi ya talc (kiungo hicho) na kansa ya kizazi ni sawasawa na mtu anayepinga hadharani uhusiano kati ya uvutaji sigara na kansa’.
Gazeti hili lilikwenda hadi ofisini kwa Mkemia Mkuu wa serikali ili kutaka kujua kama wana taarifa hizo, lakini ofisa aliyeomba hifadhi ya jina lake kwa vile siyo msemaji, alisema kiutaratibu, kazi hiyo inapaswa kufanywa na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA).
Msemaji wa Mamlaka hiyo, Gaudensia Simwanza alikiri kusajiliwa kwa vipodozi hivyo hapa nchini, lakini akasema bado hawana taarifa za kuwepo kwa watu walioathirika kutokana na matumizi ya poda hizo.
“Dawa ambazo zimesajiliwa hapa kwetu zinatokea Afrika Kusini na Ufaransa, hazitoki Marekani. Kabla ya kusajili, huwa tunafanya mawasiliano na mamlaka husika huko inakotoka (FDA) ambao wanatueleza wamepaki kiasi gani na ubora wake.
“Tunaisajili dawa baada ya kupokea banchi ya kwanza, sasa baada ya hapo mwagizaji anaendelea kuileta tu, sasa kwa maelezo yako, itabidi tuingie kazini kuangalia kama bidhaa ina ubora unaotakiwa au la, baada ya hapo tutakuwa na la kusema,” alisema.
Alisema watakusanya upya sampo za bidhaa hizo na kuzipeleka maabara ili zichunguzwe kwa mara nyingine. Endapo zitakutwa na madhara zitapigwa marufuku na pia kuwasiliana na taasisi husika Marekani ili kuwataarifu juu ya hilo pamoja na kuwasiliana na kiwanda kinachozalisha bidhaa hizo.
Jere Beasley, ambaye ni wakili wa familia ya Fox, alisema kampuni hiyo ilitambua kuwa inawaongopea wateja wake na mamlaka zinazohusika na vipodozi, wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Msemaji wa kampuni hiyo, Carol Goodrich, alionyesha masikitiko yake kwa hatua hiyo, akisema kwa miaka yote, walitambua kuwa ni jukumu lao kuhakikisha afya na usalama wa walaji wa bidhaa zao.
“Tunaumia pamoja na familia ya mlalamikaji, lakini siku zote tuliamini bidhaa zetu ni bora kutokana na ushahidi wa kisayansi.”
Ushahidi wa kisayansi unaoonyesha kiungo kinachosababisha kansa katika vipodozi hivyo siyo jambo la kificho, kwani kimemo kimojawapo kilichopatikana kutoka kwa mshauri wa kitaalamu aliyeajiriwa na kampuni hiyo kilisema ‘mtu yeyote atakayepinga uhusiano wa matumizi ya talc (kiungo hicho) na kansa ya kizazi ni sawasawa na mtu anayepinga hadharani uhusiano kati ya uvutaji sigara na kansa’.
Gazeti hili lilikwenda hadi ofisini kwa Mkemia Mkuu wa serikali ili kutaka kujua kama wana taarifa hizo, lakini ofisa aliyeomba hifadhi ya jina lake kwa vile siyo msemaji, alisema kiutaratibu, kazi hiyo inapaswa kufanywa na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA).
Msemaji wa Mamlaka hiyo, Gaudensia Simwanza alikiri kusajiliwa kwa vipodozi hivyo hapa nchini, lakini akasema bado hawana taarifa za kuwepo kwa watu walioathirika kutokana na matumizi ya poda hizo.
“Dawa ambazo zimesajiliwa hapa kwetu zinatokea Afrika Kusini na Ufaransa, hazitoki Marekani. Kabla ya kusajili, huwa tunafanya mawasiliano na mamlaka husika huko inakotoka (FDA) ambao wanatueleza wamepaki kiasi gani na ubora wake.
“Tunaisajili dawa baada ya kupokea banchi ya kwanza, sasa baada ya hapo mwagizaji anaendelea kuileta tu, sasa kwa maelezo yako, itabidi tuingie kazini kuangalia kama bidhaa ina ubora unaotakiwa au la, baada ya hapo tutakuwa na la kusema,” alisema.
Alisema watakusanya upya sampo za bidhaa hizo na kuzipeleka maabara ili zichunguzwe kwa mara nyingine. Endapo zitakutwa na madhara zitapigwa marufuku na pia kuwasiliana na taasisi husika Marekani ili kuwataarifu juu ya hilo pamoja na kuwasiliana na kiwanda kinachozalisha bidhaa hizo.
Note: Only a member of this blog may post a comment.