Wednesday, March 9, 2016

Anonymous

RICHIE Alivyowasotesha Mastaa Airport!

RICHIE (4)
Na Richard Bukos, Risasi Mchanganyiko
STAA wa filamu za Kibongo aliyeshinda tuzo katika African Magic Viewers Choice Awards ‘AVCA’ katika kipengele cha Filamu Bora ya Mwaka kupitia Filamu ya Kitendawili, Single Mtambalike ‘Richie’ mwishoni mwa wiki akiwasotesha vilivyo mastaa waliokwenda kumpokea ndani ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar alipokuwa akirejea kutoka Lagos, Nigeria.
Tukio hilo la kumpokea lilifanyika usiku wa Jumapili iliyopita ambapo mastaa kibao walikwenda ‘airport’ kumpokea Richie na kujikuta wakimsubiri kwa muda mrefu.
RICHIE (3)
Kwa mujibu wa kiongozi mmoja wa wasanii ambaye hakutaka jina lake litajwe, Richie na wenzake walitakiwa kuwasili uwanjani hapo majira ya saa nne usiku, lakini waliwasili saa saba usiku jambo ambalo liliwachosha baadhi ya mastaa waliokuwa wakiwasubiri kwa hamu kubwa.

“Yaani Richie ametusotesha kweli maana alisema watawasili kuanzia saa nne lakini angalia mpaka saa saba hii ndiyo wanafika, ukweli tumechoka lakini tunampongeza kwa sababu amerudi na tuzo kwani hii ni sifa kubwa kwetu waigizaji wa Kibongo,” alisema kiongozi huyo.
RICHIE (2)
Baada ya kuwasili shamrashamra zilishika kasi huku mastaa mbalimbali na wadau wa filamu wakiserebuka kwa staili ya kumwaga razi na kuwaacha midomo wazi raia wa kigeni waliokuwa uwanjani hapo. Miongoni mwa mastaa waliofika kumpokea Richie uwanjani hapo ni Ahmed Ulotu ‘Mzee Chilo’ Jacob Steven ‘JB’ Faiza Ally, Suzan Lewis ‘Natasha’ Kulwa Kikumba ‘Dude’, Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Simon Mwakifwamba na wengine wengi.

Richie akiwa na tuzo yake mkononi alichomoza kwenye mlango wa abiria wanaowasili mishale ya saa saba za usiku ambapo mkewe, Asha Salehe, alishindwa kujizua na kumrukia kama anapiga mbizi na kumchum, kisha kumvalisha shada na baadaye tukio la kulishana keki iliyoandaliwa na TAFF lilifuata kwa watu mbalimbali.

Akizungumza kwa furaha uwanjani hapo, Richie aliwashukuru wote waliofika kumpokea muda huo na kuwaambia kuwa kitendo hicho kimemuongezea faraja na kumpa ari ya kujituma zaidi.
Aidha alisema Watanzania sasa wameshajitambua na kuondokana na dhana potofu ya kizamani kuwa mabingwa wa kuigiza filamu katika Bara la Afrika ni Wanigeria na mataifa mengine ya magharibi.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.