Msanii wa bongo fleva,Harmonize ambaye ameachia video mpya ya bado amedai kuwa alitokwa na machozi baada ya kuona kile kipande cha kwanza cha kwenye video yake pale anapomwona mpenzi wake na mtu mwingine.
Msanii huyo ameweka kipande hicho kutoka kwenye video hiyo kwenye akaunti yake ya instagram na kuandika yafuatayo.. “wakati na shoot hichi kipande nilichukulia kawaida tu kutokana na stori ilivyo but baada ya kuiona video nilipotumiwa lilinitoka chozi inaumiza sanaaa kama ulisha wahi kuumizwa ushajua ninacho maanisha hasa yule uliempenda kwa dhati ungali wewe ungechukua maamuzi gani ……?? #Bado gusa link kuitazama “kama inavyoonekana kwenye picha hapo chini..

Note: Only a member of this blog may post a comment.