Na Hamida Hassan
Staa wa filamu za Kibongo, Tiko 
Hassan anatia huruma baada ya kuibuka na kusema kuwa unene unaomuandama 
unamnyima raha kwani kila kukicha anazidi kuongezeka.
Akizungumza na Ijumaa 
Tiko alisema kuwa, watu wengi wakimuona wanamshangaa mpaka anajisikia 
vibaya lakini hana njia ya kufanya ili ajipunguze kwani ameshahangaika 
kwenye majumba yote ya mazoezi ‘gym’ lakini hajafanikiwa. 
“Mimi hapa najiona nimepungua kidogo 
lakini nashangaa nikikutana na watu wananishangaa bado, najikuta nakata 
tamaa, kusema ukweli hata sijui nini kitanifanya nipungue, 
nachanganyikiwa mwenzenu,” alisema Tiko.

Note: Only a member of this blog may post a comment.