Kijana Geofrey Godian baada ya kunywa sumu.
Na Gladness Mallya, Risasi Jumamosi
DAR ES SALAAM: Kisa
kinashangaza! Kijana Geofrey Godian (28), mkazi wa Kimara-King’ong’o,
Dar amenusurika kifo baada ya kunywa sumu kisa kikiwa ni kukataliwa na
mkewe wa ndoa, Fatma Seleman (23).
Tukio hilo lilijiri wiki iliyopita
nyumbani kwa wanandoa hao, Kimara-King’ong’o, Dar ambapo Geofrey, baada
ya kutokea kutoelewana na Fatma kwa kile kilichodaiwa kuwa ana wivu
uliopitiliza, alifanya jaribio hilo la kutaka kujiua.
mke wa kijana huyo, Fatma Seleman.
Ilisemekana kwamba siku ya tukio, wawili
hao walikuwa wakigombana ambapo Fatma alimwambia Geofrey hamtaki ndipo
akaamua kumeza vidonge visivyokuwa na idadi vya malaria viitwavyo Oroda
ili afe.
Ilielezwa kuwa baada ya kunywa vidonge
hivyo, hali yake ilikuwa mbaya, akawa anatokwa mapovu mdomoni ambapo
mdogo wake, Pius Godian alimpa huduma ya kwanza kwa kumnywesha maziwa
‘freshi’ ndipo akaanza kutapika mfululizo.
Ilisemekana
kwamba, huku akiwa hajiwezi, alikimbizwa kwenye Hospitali ya Palestina,
Sinza jijini Dar, baada ya kupewa hati ya matibabu ya polisi (PF-3)
kutoka Kituo cha Polisi cha Kimara-Mwisho ambapo alipatiwa matibabu na
kupata ahueni.
Akizungumza na mwanahabari wetu, Fatma
alisema kuwa yeye na Geofrey wana miaka sita kwenye ndoa na wamejaliwa
kupata mtoto mmoja wa kike mwenye umri wa mwaka mmoja lakini mumewe huyo
amekuwa na wivu uliopitiliza huku mara kwa mara wakiwa na migogoro
ndani ya nyumba kutokana na mwanamke ambaye alizaa na jamaa huyo kabla
hawajaoana kumfanyia fujo kila wakati.
“Kuna
mwanamke alizaa na mume wangu kabla hatujaoana, sasa amekuwa
akinitukana na kunifanyia fujo kwa kushirikiana na marafiki zake kila
wanaponiona. Pia bado wana mawasiliano mazuri, sasa ni bora aendelee na
huyo na mimi nimrudie mwanaume wangu wa zamani niliyeachana naye
niendelee naye maana nimechoka,” alisema Fatma.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa
Kimara-King’ongo, Demetrius Mapesi alithibitisha kutokea kwa tukio hilo
ambapo alisema kuwa alifanya kazi yake ipasavyo ikiwa ni pamoja na kutoa
taarifa polisi na mke wa Geofrey kufika kituoni kwa ajili ya mahojiano.
“Nilimsikiliza
mke wa Geofrey na baadaye niliwaacha waende polisi kwa ajili ya PF-3
(fomu ya matibabu) na kupatiwa matibabu kwenye Hospitali ya Palestina
(Sinza) hadi akapona na mke kutoa maelezo Kituo cha Polisi cha
Kimara-Mwisho,” alisema Mapesi na kuongeza kuwa Geofrey itabidi akajibu
shitaka la kutaka kujiua.

Note: Only a member of this blog may post a comment.