Wednesday, December 2, 2015

Anonymous

MAMBO MUHIMU Usiyoyajua Kuhusu Mwanamke wa Kwanza Kuupata Ubunge 2015 Mkoa wa Mara…(Audio)

Kwa zaidi ya miaka hamsini jimbo la Tarime mkoa wa Mara limeongozwa na Wanaume kwa ngazi ya Ubunge , sasa time hii jimbo limeweka historia ya kuongozwa na Mwanamke Ester Matiko.
Akiongea Exclusive Interview na ripota wa millardayo alisema..’Kwa upande wa Tarime kwa maana ya Ubunge hakuna Mwanamke aliyewahi kuchaguliwa kuongoza wana Tarime mimi  ndio wa kwanza maana nasema wamenipa heshima kubwa sana heshima ambayo kwakweli nitafanya kila ninaloweza kuhakikisha kwamba natumia nafasi yangu ya Ubunge kusimamia Serikali kuhakikisha kwamba inatimiza wajibu wa kuwatumikia watanzania‘ – Ester Matiko
IMG_20151201_193139-1 (1)
Tofauti kubwa ni kwamba nimechaguliwa na wanatarime sasa hivi nawajibika moja kwa moja kwa wananchi wa Tarime tofauti iliyopo ni kwamba mwanzoni nilikuwa natumikia wananchi wa  mkoa wa Mara kwa maana ya majimbo 7 ambayo yamekuwa 10 sasa hivi nimekuwa mbunge wa Tarime wenye kata 8  na maana nawajibika kuwatumikia moja kwa moja wananchi wa Tarime mjini’ – Ester Matiko
 Unaweza ukabonyeza play kumsikiliza Ester Matiko

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.