Sunday, November 8, 2015

Anonymous

MBWANA SAMATTA Hakunaga! Full Time ya Fainali ya TP Mazembe Vs USM Alger Hii Hapa,Samatta Kwenye HeadlinesTena…

Licha ya kuwa Jumapili ya November 8 kuna michezo kadhaa inapigwa barani Ulaya ila mchezo wa fainali ya pili ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya ndio mchezo uliyokuwa umevuta hisia za watu wengi barani Afrika hususani Tanzania ambao waliokuwa wanasubiri kuwaona nyota wao Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wakiweka rekodi katika fainali hizo.
IMG_20151108_181338
TP Mazembe ilicheza mchezo huo wa pili ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa goli 2-1 katika mchezo wa kwanza, huku ikiwa na rekodi ya kutwaa taji hilo kwa mara ya mwisho mwaka 2010 na mastaa waliotwaa taji hilo katika mwaka huo wamebakia watano pekee kikosini Given Sunguluma, Robert Mutebe Kidiaba, Aime BakulaJoel Kimwaki na Jean Kasusula.
IMG_20151108_181407
Mtanzania Mbwana Samatta ambaye kabla ya mchezo huo kuchezwa alikuwa akihitaji goli moja pekee ili aweze kuweka rekodi ya kuwa mfungaji bora wa michuano hiyo kwani alikuwa sawa na mshambuliaji wa klabu ya Al Merreikh Bakri Abdel Kader Babeker wote wakiwa na jumla ya goli 6.
IMG_20151108_181434
Mchezo umemalizika kwa TP Mazembe kuibuka na ushindi wa jumla ya goli 2-0, kwa mara nyingine tena Mbwana Samatta amefanikiwa kufunga goli kupitia mkwaju wa penati baada ya Roger Assale kufanyiwa faulo dakika ya 74, USM Alger wakiwa katika jitihada za kusaka goli Mbwana Samatta alipata mpira kutokea kati ya uwanja na kukimbia nao hadi golini Roger Assale akapachika goli la pili na kuifanya TP Mazembe ichukue Kombe la Ligi ya Mabingwa Afrika kwa mwaka 2015.
IMG_20151108_190505
Unataka kutumiwa MSG za

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.