Monday, October 12, 2015

Anonymous

Vanessa Mdee Awashauri Wasanii Kuwekeza Kwenye Muziki Kama Yeye, Diamond na Ommy Dimpoz

Hii itakuwa ni wiki nzuri sana kwa Vanessa Mdee ambaye weekend iliyopita alifanikiwa kushinda tuzo ya Afrimma huko Dallas, Marekani pamoja na kuachia wimbo mpya ‘Never Ever’ na video yake.

Vee Money ambaye amewashinda Victoria Kimani, Juliana Kanyomozi na Khadija Kopa kwenye kipengele cha ‘Best Female East Africa’, ametoa ushauri kwa wasanii wengine wa Tanzania kufata mifano waliyoionesha yeye, Diamond pamoja na Ommy Dimpoz kwa kuwekeza kwenye muziki wao ili wapate mafanikio.

Vanessa ambaye video yake mpya imefanyika Afrika Kusini na kuongozwa na Justin Campos wa kampuni ya Gorilla Films, amesema, “Wasanii wengine pia wachukulie mfano wa Diamond wa Ommy wa Vanessa wa kuwekeza kwenye muziki wasiogope”
Pia amewashauri wasanii wa kike kujitokeza zaidi kutokana na uwepo wa wasanii wachache wa kike kulinganisha na idadi ya wasanii wa kiume.
Vee pia amewashukuru wote waliomsupport hadi kushinda tuzo hiyo ambayo ni tuzo yake ya pili ya nje ya Tanzania

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.