Mrisho Mpoto ameendelea kujivunia kutembea peku na kudai kuwa ni njia nzuri ya kujiongezea miaka mingi ya kuishi.
“Nimeshajibu hili swali mara milioni,” alisema Mrisho baada ya kuulizwa na Global TV sababu ya kutembea peku.
“Ili uwe na akili lazima ukanyage chini. Unajua ili uishi muda mrefu,
hili ni kosa kubwa la kiufundi ndIo maana watu wanakufa haraka na ndio
maana watu akili hawana kwa sababu watu wanakosa connection ya mwili na
udongo. Tunasema kuconnect doti kuna mahusiano makubwa kati ya ardhi ya
mwili wako. Ukuaji wako unategemea na nature tuliyonayo, hewa
unayotumia, maji pamoja na udongo. Kwahiyo kuna nguvu kubwa ambayo ipo
chini ya udongo.”

Note: Only a member of this blog may post a comment.