Monday, October 26, 2015

Anonymous

HALI ILIVYOKUWA KATIKA MAENEO MBALIMBALI MKOANI RUVUMA WAKATI WA UPIGAJI KURA

Jenister Mhagama mgombea ubunge Jimbo la Peramiho akiwa katika kituo cha kupigia kura. Chekechea Namba 1, kijiji cha Parango
WAPIGA KURA wa majimbo ya Peramiho na Songea Mjini wamejitokeza kwa wingi kwenye vituo vyao vya kupigia kura za Urais,Ubunge na Udiwani na wengine wamekesha kwenye vituo vya misufini namba 1 na namba 2 vyao vya kupigia kura kwa lengo la kuwahi foleni ya kupiga kura huku kasoro ndogo ndogo zikijitokeza lakini bila kuathiri zoezi zima la upigaji kura

Akizungumza na waandishi wa habari Msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Peramiho ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Vijijini, sisbert Valentine Kaijage alisema kuwa waliojiandisha kwenye jimbo hilo ni 67,334 ambapo idadi ya vituo vya kupigia kura ni 195

Kaijage alisema kuwa kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 wilaya ya Songea Vijijini ina idadi ya wakazi 133024 na kwamba vifaa vya kupigia kura vilishaperekwa kwenye vituo kwa wakati na changamoto ambayo imejitokeza kwenye vituo hivyo ni baadhi ya watu ambao walijiandisha kwenye majimbo ya uchaguzi wakiwemo wafanyakazi na wanavyuo nao kutaka kupiga kura

Kwa upande wake Msimamizi Msaidizi wa uchaguzi Jimbo la Songea Mjini Emmanuel Kibona kuwa kumejitokeza kasoro za Askari Mgambo kutokuwahi kwenye vituo vya kupigia kura, baadhi ya wanasiasa kuvaa sare za vyama vyao hali ambayo ilitaka kuleta taaruki, makarani kuendesha shughuli polepole na kusababisha wapigakura kulalamika
Mgombea ubunge Songea mjini kwa tiketi ya CDM Joseph Fuime
Akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kupiga kura kwenye kituo cha Shuleni A kata ya Likuyufusi Mgombea Ubunge wa Chama cha Mapinduzi Jimbo la Songea Mjini Leonidas Gama alisema kuwa ameridhishwa na hali ya upigaji kura kwani umekuwa huru na haki
Gama alisema kuwa tume imetenda kazi yake vizuri kwa kuhakikisha vifaa vyote muhimu vya kupigia kura vimefikishwa kwenye vituo kwa wakati na wapigakura wameanza muda muafaka kutumia haki yao ya kikatiba ya kushiriki kupiga kura za ubunge, urais na Udiwani

Naye Mgombea Ubunge wa Ccm Jimbo la Peramiho Jenista Mhagama mara baada ya kupiga kura katika kituo cha kupigia kura cha Chekechea namba moja kilichopo katika kijiji cha Parangu nje kidogo ya mji mdogo wa Peramiho alisema kuwa anaamini kuwa wananchi wanaendelea kupiga kura bila kuwepo kwa usumbufu wowote

Mhagama alisema kuwa wananchi wameonyesha kuwa na imani kubwa na tume ya uchaguzi kwani hakuna mahala ambapo kumekuwa na dosari kutokana na uzembe au udhaifu wa tume hiyo hali ambayo inaendelea kuufanya uchaguzi huo kuwa huru na haki

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Ruvuma ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa huo Said Thabit Mwambungu alisema kuwa mkoa wa Ruvuma una majimbo 9 na kwenye majimbo yote 9 ya uchaguzi katika mkoa huo vifaa vya kupigia kura vilipelekwa kwa wakati na wale wote ambao walithubutu kuhujumu uchaguzi huo walichukuliwa hatua kali za kisheria

Mwambungu alisema kuwa katika Jimbo la Namtumbo kuna kata mbili uchaguzi wa udiwani umeahirishwa kwa makubaliano na Tume ya Uchaguzi kutokana na makosa yaliyojitokeza na wagombea wanafasi hizo kwenye kata hizo wamekubali uamuzi huo na kwamba katika kata hizo kura ya ubunge na urais zinaendelewa kupigwa huo

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.