
Jenister Mhagama mgombea ubunge Jimbo la Peramiho akiwa katika kituo cha kupigia kura. Chekechea Namba 1, kijiji cha Parango 
 WAPIGA KURA wa majimbo ya Peramiho na Songea Mjini wamejitokeza kwa 
wingi kwenye vituo vyao vya kupigia kura za Urais,Ubunge na Udiwani na 
wengine wamekesha kwenye vituo vya misufini namba 1 na namba 2 vyao vya 
kupigia kura kwa lengo la kuwahi foleni ya kupiga kura huku kasoro ndogo
 ndogo zikijitokeza lakini bila kuathiri zoezi zima la upigaji kura
Akizungumza
 na waandishi wa habari Msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Peramiho ambaye 
pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Vijijini, sisbert 
Valentine Kaijage alisema  kuwa waliojiandisha kwenye jimbo hilo ni 
67,334 ambapo idadi ya vituo vya kupigia kura ni 195
Kaijage
 alisema kuwa kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012  
wilaya ya Songea Vijijini ina idadi ya wakazi 133024 na kwamba vifaa vya
 kupigia kura vilishaperekwa kwenye vituo kwa wakati na changamoto 
ambayo imejitokeza kwenye vituo hivyo ni baadhi ya watu ambao 
walijiandisha kwenye majimbo ya uchaguzi wakiwemo wafanyakazi na 
wanavyuo nao kutaka kupiga kura
Kwa
 upande wake Msimamizi Msaidizi wa uchaguzi Jimbo la Songea Mjini 
Emmanuel Kibona kuwa kumejitokeza kasoro za Askari Mgambo kutokuwahi 
kwenye vituo vya kupigia kura, baadhi ya wanasiasa kuvaa sare za vyama 
vyao hali ambayo ilitaka kuleta taaruki, makarani kuendesha shughuli 
polepole na kusababisha wapigakura kulalamika 
 
 
Mgombea ubunge Songea mjini kwa tiketi ya CDM Joseph Fuime 
 Akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kupiga kura kwenye 
kituo cha Shuleni A kata ya Likuyufusi Mgombea Ubunge wa Chama cha 
Mapinduzi Jimbo la Songea Mjini Leonidas Gama alisema kuwa ameridhishwa 
na hali ya upigaji kura kwani umekuwa huru na haki
Gama
 alisema kuwa tume imetenda kazi yake vizuri kwa kuhakikisha vifaa vyote
 muhimu vya kupigia kura vimefikishwa kwenye vituo kwa wakati na 
wapigakura wameanza muda muafaka kutumia haki yao ya kikatiba ya 
kushiriki kupiga kura za ubunge, urais na Udiwani
Naye
 Mgombea Ubunge wa Ccm Jimbo la Peramiho Jenista Mhagama mara baada ya 
kupiga kura katika kituo cha kupigia kura cha Chekechea namba moja 
kilichopo katika kijiji cha Parangu nje kidogo ya mji mdogo wa Peramiho 
alisema kuwa anaamini kuwa wananchi wanaendelea kupiga kura bila kuwepo 
kwa usumbufu wowote
Mhagama
 alisema kuwa wananchi wameonyesha kuwa na imani kubwa na tume ya 
uchaguzi kwani hakuna mahala ambapo kumekuwa na dosari kutokana na 
uzembe au udhaifu wa tume hiyo hali ambayo inaendelea kuufanya uchaguzi 
huo kuwa huru na haki
Kwa
 upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Ruvuma 
ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa huo Said Thabit Mwambungu alisema kuwa mkoa 
wa Ruvuma una majimbo  9 na kwenye majimbo yote 9 ya uchaguzi katika 
mkoa huo  vifaa vya kupigia kura vilipelekwa kwa wakati na wale wote 
ambao walithubutu kuhujumu uchaguzi huo walichukuliwa hatua kali za 
kisheria
Mwambungu
 alisema kuwa katika Jimbo la Namtumbo kuna kata mbili uchaguzi wa 
udiwani umeahirishwa kwa makubaliano na Tume ya Uchaguzi kutokana na 
makosa yaliyojitokeza na wagombea wanafasi hizo kwenye kata hizo 
wamekubali uamuzi huo na kwamba katika kata hizo kura ya ubunge na urais
 zinaendelewa kupigwa huo 

Note: Only a member of this blog may post a comment.