Thursday, September 10, 2015

Anonymous

KIMENUKA MBAYA! Msanii MAFUFU wa BongoMovies Ashushiwa Kichapo Heavy na Mkewe!

KIPIGO! Licha ya kujulikana na kuogopeka kwa ukorofi na ubabe uliopitiliza, muigizaji wa filamu za Kibongo, Jimmy Mafufu, amechezea kichapo kutoka kwa mkewe wa ndoa, Salma Mafufu kwa kile kilichoelezwa kuchelewa kurudi nyumbani.
‘Akiteta’ na mwandishi wetu hivi karibuni, mmoja wa marafiki wa karibu na Mafufu, ambaye anaishi mtaa mmoja na wanandoa hao, alisema tukio hilo la fedheha lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita majira ya  saa 3 usiku na kuzua ‘mtiti’ mkali. 

“Mafufu amepangiwa na mkewe kurudi nyumbani mwisho saa moja sasa siku hiyo alinipigia simu na kuniomba niende nyumbani kwake, nilipofika nikamkuta akigugumia maumivu kwenye mkono wa kushoto na kudai kuwa alipigwa kwa kitu kizito na mkewe baada ya kuchelewa kurudi,” alisema ‘yuda’ huyo wa Mafufu.
Baada ya kupata umbea huo, mwandishi wetu  alimtafuta Mafufu ambapo alisema ni kweli alipigwa na mkewe na alipata mshtuko kidogo kwenye mkono kwani alipigwa na kipande cha mti ila ugomvi ndani ya ndoa ni kitu cha kawaida.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.