KIPIGO! Licha ya kujulikana na kuogopeka kwa ukorofi na ubabe 
uliopitiliza, muigizaji wa filamu za Kibongo, Jimmy Mafufu, amechezea 
kichapo kutoka kwa mkewe wa ndoa, Salma Mafufu kwa kile kilichoelezwa 
kuchelewa kurudi nyumbani.
‘Akiteta’
 na mwandishi wetu hivi karibuni, mmoja wa marafiki wa karibu na Mafufu,
 ambaye anaishi mtaa mmoja na wanandoa hao, alisema tukio hilo la 
fedheha lilijiri mwishoni mwa wiki iliyopita majira ya  saa 3 usiku na 
kuzua ‘mtiti’ mkali. 
“Mafufu amepangiwa na mkewe kurudi nyumbani mwisho saa moja sasa siku
 hiyo alinipigia simu na kuniomba niende nyumbani kwake, nilipofika 
nikamkuta akigugumia maumivu kwenye mkono wa kushoto na kudai kuwa 
alipigwa kwa kitu kizito na mkewe baada ya kuchelewa kurudi,” alisema 
‘yuda’ huyo wa Mafufu.
Baada ya kupata umbea huo, mwandishi wetu  alimtafuta Mafufu ambapo 
alisema ni kweli alipigwa na mkewe na alipata mshtuko kidogo kwenye 
mkono kwani alipigwa na kipande cha mti ila ugomvi ndani ya ndoa ni kitu
 cha kawaida.
 

 
 
 
 
Note: Only a member of this blog may post a comment.