Thursday, September 10, 2015

Anonymous

Ushirikina Wamkimbiza JACK wa Maisha Plus Kwenye Nyumba

IMG_9247

Jack Dustan.
Imelda Mtema
MWANADADA aliyejipatia jina kupitia Shindano la Maisha Plus Season 11, Jack Dustan amejikuta akiihama nyumba aliyokuwa amepanga maeneo ya  Shekilango jijini Dar, kwa madai kwamba ilikuwa na nguvu za kishirikina ‘mapepo’.
Akistorisha na Amani hivi karibuni,  Jack alisema nyumba hiyo alipanga na kukaa kama wiki moja tu lakini akawa anakumbwa na mambo ya ajabu kwani kuna wakati alikuwa akijikuta amelala nje kwenye kizingiti cha mlango wa chumbani kwake. 

Aliendelea kusema siku aliyoamua kuondoka bila kubeba vitu vyake vya ndani ni baada ya usiku kupigwa sana vibao na kuamriwa kutoa pombe alizoweka kwenye kabati ili awe salama.
“Ukweli sijabeba kitu  chochote, nilitimua zangu usiku uleule na kwenda kulala kwa rafiki yangu  na nimetafuta nyumba nyingine-,” alisema Jack.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.