Klabu ya Real Madrid ya Hispania
ni klabu ambayo inasifika kwa kupenda kununua wachezaji kwa gharama ya
juu maadam iwe inamuhitaji basi itatoa fedha ili kukamilisha usajili
wake. Headlines ambayo ipo katika vyombo vya habari ni kuhusiana
na klabu ya Paris Saint Germain ya Ufaransa ambayo inahusishwa kutaka kumsajili Cristiano Ronaldo.
Kabla ya dirisha la usajili kufungwa klabu ya PSG ilikuwa ikihusishwa kutaka kumsajili Cristiano Ronaldo ila klabu ya Real Madrid ya Hispania hawakuwahi kutoa majibu yoyote kuhusu mpango huo. September 10 kupitia kwa Rais wa klabu ya Real Madrid Florentino Perez amesema kama PSG wanamuhitaji Ronaldo hakuna shida ila waje na pound milioni 728.
“Kama PSG
wanamuhitaji Cristiano Ronaldo ni kazi rahisi na wala hakuna tatizo,
wanatakiwa kulipa pound milioni 728, hakuna nabii katika mchezo wa mpira
wa miguu yoyote anaweza kuuzwa lakini hatuhitaji kumuuza mwaka 2016
kwani bado ana mkataba wa miaka mitatu umebakia”>>> Florentino Perez
Cristiano Ronaldo alijiunga na klabu ya Real Madrid mwaka 2009 akitokea klabu ya Manchester United ya Uingereza kwa dau la pound milioni 80, dau ambalo liliweka rekodi ya dunia, ila klabu ya PSG ipo tayari kumsajili mshambuliaji huyo kwa dau la pound milioni 87, hii ilikuwa kabla ya dirisha la usajili kufungwa.

Note: Only a member of this blog may post a comment.