Friday, September 4, 2015

Anonymous

PICHAZ: Uliipata hii ya David James kupewa adhabu na kocha ya kuendesha gari ya matairi matatu? kilichofuata….


Wazungu wana vitu vingi sana vya kushangaza tofauti na sisi kwetu Afrika, wapo wazazi wa kizungu wana tabia ya kutumia mfumo wa kidemokrasia ili kumkanya mtoto. Katika mpira wa miguu kocha ni kama baba katika timu anapaswa kusikilizwa.


Hii ni stori ya nyuma kidogo iliwahi kuandikwa mwezi August mwaka 2013 na mtandao wa tsmplug.com, kocha wa zamani wa klabu ya Portsmouth ya Uingereza Tony Adams, aliwahi kumpa adhabu golikipa wa timu hiyo David James ya kuendesha gari ya matairi matatu kwa sababu hakuwa akifanya vizuri mazoezini.

Hapa ilikuwa kabla ya David James kulifanyia matengenezo
Baada ya kumpa adhabu hiyo, James alikubali kuitumia gari hiyo ya matairi matatu cha kushangaza baada ya kuondoka nayo akaenda kuifanyia matengenezo na kuifanya iwe ya matairi matano licha ya kuwa Tony Adams alimpa gari hiyo kama adhabu kwake.

Baada ya kulifanyia matengenezo

stori kwa mujibu wa tsmplug.com

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.