Friday, September 4, 2015

Anonymous

MUNGU Mkubwa!

gonjwa2
Na Makongoro Oging’
Faiza Masaka Paga (23) mkazi wa Chanika, Msumbiji, Wilaya ya Ilala jijini Dar, ambaye alikuwa akisumbuliwa na uvimbe kwa muda mrefu hatimaye amefanyiwa upasuaji na madaktari bingwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wiki iliyopita.
GONJWA (1) 
Faiza aliliambia gazeti hili kuwa kutokana na kufanyiwa upasuaji kwa mafanikio makubwa, alitolewa uvimbe uliokuwa na kilo sita na nusu mwilini mwake.
GONJWA (2) 
Alisema anawashukuru wananchi wote waliomchangia fedha baada ya kuandikwa habari yake katika gazeti hili tolea namba 915 la Juni 23 hadi 25 mwaka huu likiwa na kichwa cha habari: GONJWA LA AJABU,  hali iliyosababisha wananchi kujitokeza kwa wingi kumchangia.
GONJWA (3)“Nawashukuru sana pia madaktari na wauguzi ambao muda wote walikuwa karibu nami katika kunihudumia,” alisema.
Faiza  ni yatima sasa anauguza kidonda, anasaidiwa na msamaria mwema mwanamke ambaye ana kipato cha chini isitoshe ana watoto wawili ambao afya zao siyo nzuri.
gonjwa 
Pia bado anatakiwa kwenda Hospitali ya  Muhimbili kila wiki mara moja ambapo anatakiwa kukodisha teksi kwenda na kurudi lakini fedha hana.
Kwa yeyote anayependa kumsaidia binti huyu awasiliane naye kwa namba ya simu : 0787 853153, 0654 187240 au 0717 260769.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.