Saturday, September 12, 2015

Anonymous

MAJONZI: Hausigeli Ajinyonga Kisa MAPENZI Mkoani Morogoro!


AJINYONGA (3)-001
Mwili wa marehemu Rehema ukiingizwa kwenye gari la polisi ili kwenda kuhifadhiwa hospitali.
Dustan Shekidele, Moro
Mfanyakazi wa ndani ‘hausigeli’ mmoja mkoani hapa aliyefahamika kwa jina moja la Rehema (16) ambaye alifanya kazi hiyo kwa wiki moja, akimshikia mwenzake aliyekwenda kijijini kwao lfakara wilayani Kilombero kumuuguza mama yake, amejifungia chumbani kisha kujinyonga kwa kutumia kanga.
AJINYONGA (4)-001Umati wa watu waliofika kushuhudia tukio hilo.
Tukio hilo la kuhuzunisha lilijiri usiku wa kuamkia juzi (Alhamisi) kwenye nyumba namba 17\l3 aliyokuwa akifanya kazi Rehema iliyopo Mtaa wa Kazingwa Kata ya Kiwanja Cha Ndege mjini hapa huku kisa kikiwa cha kusikitisha cha kimapenzi.
AJINYONGA (5)-001Gari la polisi likiwa linaondoka eneo la tukio.
Kwa mujibu wa mashuhuda, katika hali ya kushangaza, familia iliyokumbwa na mkasa huo iligoma kuhojiwa na mwandishi wetu huku wakimtaka akachukue maelezo polisi.
Baada ya wanafamilia hao kugoma, mwanahabari wetu alizungumza na mmoja wa wapangaji aliyeomba hifadhi ya jina ambaye alisimulia:
AJINYONGA (6)-001“Hapa kulikuwa na hausigeli aliuguliwa na mama yake huko lfakara, akapewa ruhusa kwa sharti la kumleta ndugu yake kumshikia nafasi.
“Kweli akamleta huyu Rehema. Cha ajabu Alhamisi, majira ya saa 1:00 asubuhi anagongewa mlango wa chumba ila hakujibu chochote.
AJINYONGA (7)-001“Tulipozunguka dirishani na kuchungulia ndipo tukamkuta  amejinyonga.”
Baadhi ya mashuhuda wengine walieleza kwamba hadi Rehema anachukua uamuzi huo inawezekana kuna mambo yalikuwa yamemfika shingoni.
AJINYONGA (1)-001“Kuna maelezo kuwa huko alikotoka amelazimishwa kuja kufanya kazi hii na alikuwa na bwana’ke ambaye walikuwa na mipango ya kuoana, sasa kalazimishwa kuja kumshikia kazi ndugu yake,” alidai mmoja wa mashuhuda.
AJINYONGA (2)-001Mwili wa marehemu rehema ukiwa umetolewa ndani naukipelekwa kwenye gari la polisi.
Kwa upande wake, mwenyekiti wa mtaa huo, Mohamed Mbega alithibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo aliita polisi waliofika na kuuchukua mwili wa marehemu Rehema kwa uchunguzi zaidi na taratibu za mazishi.
Katika tukio hilo lililokusanya umati mkubwa, Rehema hakuacha ujumbe wowote kwani begi lake lilikaguliwa na halikuwa na ujumbe zaidi ya nguo zake hivyo kumfanya bosi wake kuchanganyikiwa.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.